Wednesday, September 8, 2010

SHUKRANI

Natanguliza shukrani zangu za dhati kwa wale wote walioniandikia e-mail kunitia MOYO na hata kuleta maombi yao kwangu nawashukuru sana. Kusema kweli  MAOMBI YOTE nitayafanyia kazi na naamini Mungu wangu ninayemtumainia atawajibu kila mtu hitaji la MOYO wake, wenye magonjwa hakika mtaponywa na hakuna kulemewa tena na mizigo. Wengi mmeomba nisipublish maombi yenu nami naahidi kutokufanya hivyo (yote mliyoandika ni siri), japo kwa wale ambao watakubali kutoa ushuhuda wanakaribishwa kwa sababu unapotoa ushuhuda unamwaibisha shetani na vile vile unamfungua na mwingine ambaye alikuwa anatatizo kama lako naye anapata kufunguliwa katika vifungo mbalimbali walivyofungwa. (majina hayatatajwa hivyo usiwe na hofu). Nitakuwa natoa mistari ya Biblia ya kusoma kila siku vile vile kwa wale tunaowasiliana kwa njia ya e-mail nitakupatia kulingana na hitaji lako.

Tusikate tamaa kwani tumaini la Bwana lipo na hakuna lisilowezekana na lisilo na jawabu chini ya jua hili yote yawezekana kwake yeye yule aaminie. HAKIKA UTASHINDA KWANI HAKUNA JARIBU LISILOKUWA NA MLANGO WA KUTOKEA. BARIKIWA  SANA NA BWANA.

No comments: