Sunday, January 30, 2011

USHUHUDA

Namshukuru Mungu sana kwa kunipa mafunuo ya kuanzisha hii Blog kwani toka nianzishe nimeona jinsi Mungu anavyotenda ndani ya maisha yangu na pia kunipa kibali mbele za watu kwani nimefanikiwa kukutana na watu kupitia blog hii ambao hapo kabla nilikuwa siwafahamu na kujua kuwa bado kuna watu wana kiu ya kumjua Mungu sana na wengi wako kwenye vifungo.
Nimepata email kadha wa kadha za watu kuomba maombi nami nimefanya hivyo kwa uweza wa Roho mtakatifu na usaidizi wake. Lakini hivi karibuni nimepata maombi ya kipekee kutoka katika nchi moja huko Africa. Huyu ni mtumishi wa Mungu ambaye analo kanisa lake lenye watu thelathini, yeye badala ya kuomba maombi aliomba asaidiwe Biblia kwa ajili yake yenye Maandishi makubwa ili aweze kuwafundisha vizuri waumini wake, kwani anasema kutokana na umri alio nao kwa maana ni mtu mzima macho yake hayaoni vizuri. Nami kwa msaada wa Mungu naamini ni kwa kibali chake kumwelekeza huyu mtumishi kwangu hivyo imenipasa kufanya  hivyo na zaidi. Namshukuru Mungu kwa hili kwani siku zote nilikuwa namwomba Mungu anitumie mimi kama chombo chake sasa naamini kuwa nimefanyika chombo kwa Bwana kwa watu kupata neno lake ambalo ni muhimu katika maisha yetu sisi sote na naamini litawafungua wengi katika vifungo.

Namshukuru Mungu kwa ajili ya hili kwani naamini hizi Biblia zitawaokoa wengi ambao watalisikia neno akiwahubiria huyu mtumishi nami nitakuwa nimeishi andiko katika Yohana 15:1-2

Bwana Yesu Apewe Sifa sana sana sana. Tuzidi kupendana na Amani ya Kristo itawale mioyoni mwetu. Amen amen.

RAHA YA UWOKOVU

Ukiwa ndani ya Yesu kuna raha  mpendwa asikwambie mtu, yote yanawezekana kwa Bwana hata yale ambayo kwa akili za kibinadamu ni magumu kuwezekana ili maradi tu umwamini. "Biblia inasema hivi, yote yawezekana kwake yeye aminie". Nami na mwamini Mungu nimeuona mkono wake ndani ya maisha yangu, amani niliyonayo leo na furaha vyote nimevipata kutoka kwake yeye. Ananishindia siku hadi siku kila kitu kwangu ni shwari kwani najua ninaye mwenye uweza wote aliye mbele yangu, anayenipenda aliyenishika mkono anayeijua kesho yangu tangu nikiwa tumboni mwa mama yangu Bwana Mungu Yesu Kristo pamoja na Roho wake Mtakatifu naamini hata niacha kamwe, ananikumbatia na kunitia nguvu. Furaha, amani, utulivu, nguvu, na uweza ninavyo leo kwa sababu siku moja niliamua kuwa nataka kuwa na mshauri, mpenzi, mwalimu, kiongozi, baba Yesu Kristo ndani ya maisha yangu naye bila hiyana akanikubali akanivuta karibu nae akaniambia mwanangu karibu nyumbani hapa umefika yale uliyopitia na kuyaona hapo kabla hayatakupata tena kamwe na wala hautayaona. Kama alivyowaambia wana wake wa Israel kuwa hao Wamisri mnaowaona leo hamtawaona tena kamwe na mimi akaniambia kuwa  Wamisri waliokuwa katika maisha yangu sitawaona tena kamwe nami nina amini hivyo na zaidi. 

Wewe je unataka kuonja furaha na amani hii niliyo nayo mimi leoo?Njoo kwa Yesu leo ndugu yangu mkubali awe Bwana na Mwokozi katika maisha yako nawe utapata penzi la kweli lisilo na mawaa. Yale yote yaliomwiba kwako yatakwisha na hautayapata wala kuyaona tena.

Nampenda Yesu sana na Yeye anakupenda pia karibu upate furaha ya kweli na tufurahi pamoja.