Friday, September 24, 2010

KUHUSIANA NA EMMANUEL TV

NAJUA BAADHI YA WATANZANIA WENZANGU MNAPENDA SANA KUSIKILIZA MAFUNDISHO YA MTUMISHI WA MUNGU T. B. JOSHUA NA KITUO CHAKE CHA TELEVISION CHA EMMANUEL MNAKIPENDA SANA LAKINI SOMA HII UONE SHETANI  ANAVYOWEZA KUPENYA SEHEMU ZILE WATU WENYE KIU NAZO

Naomba uwahabarishe wadau ,Kuna matapeli wameingia nchini Tanzania ( Dar es Salaam) wanadai wao ni representatives wa T.B. Joshua wa SCOAN na Emmanueli TV. SCOAN wamekanusha kutuma representative nchini, hivyo kuweni makini. Matapeli wa aina hii wameenea duniani ambao hujipatia mali kwa jina la T.B.Joshua na Emmanuel TV.
Kwa habari zaidi angalieni Emmanuel TV au someni kwenye mtandao www.emmanueltv.com.
Asanteni na tuwe makini na hawa matapeli
(kwa hisani ya Michuzi)

TUELIMISHANE

Kusema kweli mimi wakati mwingine nashindwa kuelewa hapa naomba msaada wenu jamani kujua tofauti ya hawa wenye kazi hii na wale tunaokwenda kwa ajili ya mambo mengine mengine (wale tunaopenda kuvunja kazi zao na mipango yao katika jina la Yesu) yaani waganga wa kienyeji. Je hawa si wale wale jamani au ni sawa na hospitali kwa daktari unakwenda basi na hawa ndio jambo moja. Nina maswali mengi mno naamini na nyie ndugu mnayo tusaidiane kuelimishana pia tusisahau kuiombea nchi yetu tuwapo kwenye maombi jamani.




Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Bi.Blandina Nyoni akipata maelezo kutoka kwa mtaalam wa tiba za asili Dkt. Ahmad Darusi kuhusu namna ya kutumia Dawa aliyoitengeneza yenye uwezo wa kuwasaidia wagonjwa wa UKIMWI wakati wa sherehe za uzinduzi wa Usajili wa waganga wa Tiba za asili na Tiba mbadala leo katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es salaam.
Katibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii Bi. Blandina Nyoni akituma fomu za usajili wa waganga wa tiba za asili na tiba mbadala kwa njia ya mtandao katika mikoa yote ya Tanzania leo jijini Dar es salaam fomu ambazo zitapatikana kwenye ofisi za Halimashauri kote nchini kwa ajili ya usajili. Wanaoshudia Kulia ni Mganga mkuu wa serikali Dkt. Deo Mutasiwa na Msajili wa Tiba za Asili na Tiba Mbadala Dkt. Paul Muhani (Kushoto).

 Baadhi ya wataalam wa Tiba za asili wakiwa na dawa mbalimbali za asili walizozitengeneza tayari kwa maonyesho leo wakati wa sherehe za uzinduzi wa Usajili wa waganga wa Tiba za asili na Tiba mbadala katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es salaam.

(Hii ni kwa hisani ya blog ya Isaa Michuzi)

KUHUSU VAZI LA KWENDEA KANISANI

KUMBE LIPO JAMBO KATIKA VAZI LA KANISANI
Nimekutana na mtumishi mmoja wa Bwana dada mtanashati ambaye aliwahi kushiriki Miss Tanzania miaka ya nyuma na kwa sasa ameokoka na Bwana anamtumia tukawa tunazungumza kuhusiana na VAZI LA KWENDEA KANISANI (hii ni kutokana na post zangu za nyuma) akasema yeye ameipata hii kutoka kwa mtumishi wa Mungu mmoja ambaye alimwambia kuwa si kwamba makanisa wanakataza uvaaji wa mabinti au wamama kuvaa vimini kanisani (na makanisa mengine hata suruali kwa wanawake wanakataza) tatizo linakuwa ni kwa hao Baba zetu na kaka zetu ambao tamaa ya mwili bado kufishwa kwani wakiona wadada wamevaa namna hiyo na akiwa ibadani basi mambo ya ibada yanaishia hapo hapo inakuwa tena umempeleka sehemu nyingine kabisa na hata neno kusikiliza inakuwa ngumu. Kwa hiyo inakuwa uwepo wake ibadani siku hiyo ni ya bure hapokei kitu kabisa.
Na huyo mtumishi wa Bwana pia akatoa mfano wa akina mama/dada wengine wanaokaa viti vya mbele kabisa wengine wanajisahau sana unakuta anakaa vibaya hivyo pia inampa wakati mgumu mtumishi wa Bwana wakati yuko mbele anatoa Neno la Mungu kwani kukwambia kaa vizuri anashindwa na yeye ni mwanaume rijali basi inabidi aweke macho pembeni ili kuweza kutokuvutiwa na kuchungulia kwani anasema wao pia ni binadamu na shetani anatafuta kila njia ya kuweza kuwaangusha. "Kumwingiza mtumishi wa Mungu majaribuni ni laana kubwa tena kubwa sana."
Hivyo basi cha msingi wanachoona kinafaa kufanya ni kuwaambia wamama na wadada wavae nguo ndefu na magauni mapana au wasivae suruali kama sheria ya kanisa ili kuepusha kuwapoteza au kuwakwaza au hata kuwaingiza majaribuni baadhi ya wababa na wakaka na hata baadhi ya watumishi wawapo kwenye uwepo wa Mungu (kanisani)

Nadhani nitakuwa nimeleweka kama sivyo, namsihi Roho Mtakatifu aliye mwalimu mkuu akueleweshe.
Vazi la kanisani linatakiwa kuwa hivi wapendwa. (Haswa kwa wale wakaaji wa mbele kabisa)

Helen & Mama miezi kadhaa iliyopita Brooklyn Tabernacle tukitoka kanisani.

Mtoto wa Kifai (Matechi's la familia)
yeye hutoka hivi kwenda kanisani.

FRIENDSHIP

Friendship is not about who you have known the longest..........
but about who came and never left your side..
Four things you can't recover:
The stone.........after the throw. The word..........after it's said.
The occasion........after it's missed. The time.........after it's gone.


Knock, Knock I knocked at heaven's door this morning. God asked me...'My child, what can I do for you?' And I said, 'Father, please protect and bless the person reading this message.' God smiled and answered....'Request granted'.