Monday, November 1, 2010

JE WAJUAAA NO.6

Biblia inatuambia hivii

UPENDELEO HUDANGANYA, NA UZURI NI UBATILI. BALI MWANAMKE AMCHAYE BWANA NDIYE ANAYESIFIWA.

Haya wanawake hima hima tusijione wazuri, tusisifiwe tu kwa kuvaa mavazi yakaka vyema mwili mwetu,  kuwa na sura nzuri nk tukasahau kumcha Bwana kwani sifa yetu kuu ndio hii ya( kumcha Mungu). Kwani hata Mfalme Suleiman anasema kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa hivyo maarifa yetu yanaongezeka kwa kumcha Bwana. Na maarifa ni muhimu sana kwetu sisi kwani ni Roho ya Mungu ikiingia kwako aha wewe ni kiumbe cha tofauti mtazamo wako ni wa tofauti kabisa unaona kama Mungu aonavyo.

MSEMO! MSEMO!! MSEMOOOO NO. 4

Nimekuwa kimya kwenye msemo sana sasa naona hii ni msemo tosha kabisa.
Biblia inakuambia kwamba,
ADUI ZA MTU NI WATU WA NYUMBANI MWAKE MWENYEWE

Tafakariii

Mweleze Yesu shida yako kwani yeye anayo majibu ya maswali yako, suluhisho na pia hatima ya maisha yako anayo yeye. Usione shida ndugu kumweleza, ingia kwenye chumba chako cha siri teta naye anasikia atakupa majibu.

Ashukuriwe Mungu kwa zoezi la kupiga kura kumalizika kwa amani

Namshukuru Mungu kwa zoezi la upigaji kura nchini kwetu kwenda kwa amani. Tuzidi kuomba tusichoke kwa ajili ya matokeo yanayotangazwa nayo yamalizike kwa amani na usalama ili kusudi la uchaguzi mzima limalizike kwa utulivu na amani.

MIMI MWENYEWE LEO WAPENDWA TOKA ALIFAJIRI NIKO KWENYE TV, INTERNET NIKICHUNGULIA MATOKEO YAANI HADI NIMECHOKA YANATOKA KIDUCHU KIDUCHU NIMEFUNGUA BLOG ZOTE NA WEBSITE KARIBU ZOTE ZA TANZANIA ZA WATOA HABARI HADI NIMECHOKAAAAAA MWEE NINA KIU YA KUJUA MATOKEO KAMA NINI SIJUI HAYA TUSUBIRIE TUONE YATAKAYOJIRI

ACHA NISOME BIBLIA KWANI HII NI MUHIMU NA KIU YANGU NILITAKIWA NIIELEKEZE HUKU ZAIDI.